Ashura
aliiona siku yake kuwa ya kipekee sana mchana wa siku ile, alitamani siku kama
ile ingewai kufika kwani alikuwa akiisubiri na kuitamani kila asubuhi aliyokuwa
mbele ya dressing table kubwa chumbani kwake, hatimaye ilifika siku aliyoiota
kila usiku na kutamani iwe ndoto ya kweli. Muda wote Ashura alionekana
mchangamfu isivyo kawaida yake
‘Eh!
Shosti kulikoni mbona unatabasamu mwenyewe na hyo simu?’ aliuliza Anitha rafiki
wa Ashura ambaye pia walikuwa wakifanya kazi ofisi moja
‘Its
just nothing mamy’ alijibu Ashura kwa sauti ya kudeka huku akimgeukia Anitha
aliyekuwa akimtazama kwa mshangao
Saa
kumi jioni ndio muda wa Ashura kutoka ofisini muda ambao siku zote aliuona kama
ni mapema sana kwake kwenda nyumbani lakini leo aliuona kama ni muda
uliochelewa sana kufika, hamu yake yote ilikuwa ni kuwasiliana na ata kuonana
na Abuye kijana aliyekutana nae masaa machache yaliyopita na kubadili kabisa
mtazamo wa binti huyu. Hatimaye saa kumi ilifika Ashura haraka haraka alizima
computer kubwa iliyokuwa mbele yake huku akijisogeza ndani ya kiti cha
kuzunguka kilichiuwa a nakshi maridhawa za rangi ya silva
‘mamy
see you, I have something very important today’ aliaga Ashura huku akijiweka
sawa tayari kuelekea alipo park gari tayari kuanza safari ya kurudi nyumbani
‘its
everything fine!?’ aliuliza Anitha huku akiwa na mshangao kidogo kwani haikuwa
kawaida ya Ashura kuwahi kutoka kazini tena akiwa katika hali isiyoeleweka
‘yeah
mamy, ok bye!’ alijibu Ashura huku akionekana kutokutaka maongezi mengi
Akiwa
ndani ya gari Ashura alimpigia Abuye simu namba ikawa inatumika, alisononeka
kidogo lakini akajipa moyo akifika nyumbani atamtafuta tena. Njiani Ashura
alikuwa ni mtu mwenye furaha ya ghafla ambayo hata yeye mwenyewe alijihisi kuwa
hayupo kawaida ila kwa vile aliijua sababu hata hakuangaika kuumiza kichwa
kuifikiri ilipotoka furaha yake. Baada ya nusu saa Ashura alikuwa tayari amefia
nyumbani mawazo na akili yake yote yalikuwa kwa Abuye hakutaka kupotea kabisa
muda alifanya mambo yote yanayotakiwa kufanywa na mwanamke kasha akajipumzisha
juu ya kitanda kikubwa cha sita kwa sita.
Ashura
alichukua simu na kumpigia Abuye, baada ya sekunde chache sauti ya kiume
iliyosema ‘Allo!’ ilipenya kwenye sikio la Ashura, kimya kikapita bila kujua
ajibu nini kasha kwa uoga Ashura alijibu salamu na kumjulia hali Abuye
‘Alo!,
mambo vipi mwaya’ kwa sauti nyembamba ya upole aliuliza Ashura
‘Poa,
sista mambo?’ alijibu Abuye kwa kujiamini
‘safi
tu wangu, unapenda kuniita sista ee!’ alijibu na kuchomekea swali Ashura
‘kawaida
tu sista angu, nimeshazowea kutumia jina ilo kwa watoto wa kike’ aliendelea
Abuye
‘haha!
Eti watoto wakike, haya basi mimi nataka uchague jina la kuniita mimi, ila
tofauti na hili’ alijichekesha Ashura huku akijishaua kitandani kwake
‘ah!,
poa nitakutafutia kwanzia kesho nitakubadilishia jina’ aliongezea Abuye
‘ungependa nikuite jina gani ulipendalo?’
‘Aaa!
Mimi lolote tu zuri utakalochagua wewe’
Waliendelea
na maongezi ya hapa na pale kuweza kufahamiana zaidi kadiri maongezi
yalivyozidi ndivyo na furaha ya Ashura ilizidi kuongezeka, Ashura alimsimulia Abuye
histora yake japo kwa ufupi, huu Ashura naye akiiskiliza historia ya Abuye
ndipo aligundua kuwa Abuye alikuwa ni mwanafunzi katika moja ya vyuo jijini Dar
es Salaam akisoma shahada ya sheria. Ashura alizidi kuvutiwa zaidi na Abuye aliyeonekana
na uwezo mkubwa wa kuongea na kujiamini. ‘hakika huyu ndiye mwanaume
anayenifaa’ aliwaza Ashura wakati akimsikiliza Abuye. Baada ya maongezi ya
takribani saa nzima Abuye alimwambia Ashura kuwa anaitaji kupumzika kidogo
kwani amechoka sana na pilika pilika za siku nzima
‘Ah!
Mbona mapema sana jamani, vipi umekula kweli hata?’ aliuliza Ashura kwa unyonge
kwani stori zilikuwa zimeshamkolea
‘Nimechoka
tu Ashura, nitakula nikiamka mida ya saa mbili’ alisema Abuye huku akijua wazi
kuwa Ashura asingependa amuache peke yake
‘sawa’
alijibu Ashura kwa unyonge ‘ukiamka uni text mwaya’
‘Ok
usijali nikiamka tu utakuwa mtu wangu wa kwanza kuwasiliana naye Ashura’
alijibu Abuye kwa uchangamfu jibu lililompa matumaini Ashura
‘Ok
baadae, sleep tight’ alijibu Ashura.
Baada
ya kujibu na kukata simu ilikuwa tayari ni mida ya saa 12 na dakika saba, Abuye
alijilaza kwa uchovu haikupita muda mrefu akawa tayari ameshachukuliwa na
usingizi.
Kwa
Ashura saa 12 ulikuwa ni muda wa kuangalia habari mbali mbali za kimataifa BBC
News Channel, ila kwa siku ile aliamua kujishuhulisha na shuhuli ambazo
angezifanya saa mbili usiku ili apate uda mzuri wa kuongea na Abuye, taratibu
ratiba yake ya kila siku ilianza kubadilika japo aliona kama jambo la kawaida
tu!, muda wote aliokuwa akijishuhulisha alimuwaza Abuye, aliiwaza sauti yake
akauwaza mwili wake uliokuwa si mfupi wala si mrefu sana unaweza kuuita mwili
wa kati si mnene sana wala si mwembamba pia, Ashura alizidi kutamani siku moja
auguse japo mara moja tu!. ‘Ah! Kajialiwa sauti sawa na mwili wake, jamani
duniani kuna wanaume ma handsome adi wa sauti’ aliwaza Ashura huku akitabasamu
Inaendelea...
Ah! NIONGEZEE (2)
Ashura
aliiona siku yake kuwa ya kipekee sana mchana wa siku ile, alitamani siku kama
ile ingewai kufika kwani alikuwa akiisubiri na kuitamani kila asubuhi aliyokuwa
mbele ya dressing table kubwa chumbani kwake, hatimaye ilifika siku aliyoiota
kila usiku na kutamani iwe ndoto ya kweli. Muda wote Ashura alionekana
mchangamfu isivyo kawaida yake
‘Eh!
Shosti kulikoni mbona unatabasamu mwenyewe na hyo simu?’ aliuliza Anitha rafiki
wa Ashura ambaye pia walikuwa wakifanya kazi ofisi moja
‘Its
just nothing mamy’ alijibu Ashura kwa sauti ya kudeka huku akimgeukia Anitha
aliyekuwa akimtazama kwa mshangao
Saa
kumi jioni ndio muda wa Ashura kutoka ofisini muda ambao siku zote aliuona kama
ni mapema sana kwake kwenda nyumbani lakini leo aliuona kama ni muda
uliochelewa sana kufika, hamu yake yote ilikuwa ni kuwasiliana na ata kuonana
na Abuye kijana aliyekutana nae masaa machache yaliyopita na kubadili kabisa
mtazamo wa binti huyu. Hatimaye saa kumi ilifika Ashura haraka haraka alizima
computer kubwa iliyokuwa mbele yake huku akijisogeza ndani ya kiti cha
kuzunguka kilichiuwa a nakshi maridhawa za rangi ya silva
‘mamy
see you, I have something very important today’ aliaga Ashura huku akijiweka
sawa tayari kuelekea alipo park gari tayari kuanza safari ya kurudi nyumbani
‘its
everything fine!?’ aliuliza Anitha huku akiwa na mshangao kidogo kwani haikuwa
kawaida ya Ashura kuwahi kutoka kazini tena akiwa katika hali isiyoeleweka
‘yeah
mamy, ok bye!’ alijibu Ashura huku akionekana kutokutaka maongezi mengi
Akiwa
ndani ya gari Ashura alimpigia Abuye simu namba ikawa inatumika, alisononeka
kidogo lakini akajipa moyo akifika nyumbani atamtafuta tena. Njiani Ashura
alikuwa ni mtu mwenye furaha ya ghafla ambayo hata yeye mwenyewe alijihisi kuwa
hayupo kawaida ila kwa vile aliijua sababu hata hakuangaika kuumiza kichwa
kuifikiri ilipotoka furaha yake. Baada ya nusu saa Ashura alikuwa tayari amefia
nyumbani mawazo na akili yake yote yalikuwa kwa Abuye hakutaka kupotea kabisa
muda alifanya mambo yote yanayotakiwa kufanywa na mwanamke kasha akajipumzisha
juu ya kitanda kikubwa cha sita kwa sita.
Ashura
alichukua simu na kumpigia Abuye, baada ya sekunde chache sauti ya kiume
iliyosema ‘Allo!’ ilipenya kwenye sikio la Ashura, kimya kikapita bila kujua
ajibu nini kasha kwa uoga Ashura alijibu salamu na kumjulia hali Abuye
‘Alo!,
mambo vipi mwaya’ kwa sauti nyembamba ya upole aliuliza Ashura
‘Poa,
sista mambo?’ alijibu Abuye kwa kujiamini
‘safi
tu wangu, unapenda kuniita sista ee!’ alijibu na kuchomekea swali Ashura
‘kawaida
tu sista angu, nimeshazowea kutumia jina ilo kwa watoto wa kike’ aliendelea
Abuye
‘haha!
Eti watoto wakike, haya basi mimi nataka uchague jina la kuniita mimi, ila
tofauti na hili’ alijichekesha Ashura huku akijishaua kitandani kwake
‘ah!,
poa nitakutafutia kwanzia kesho nitakubadilishia jina’ aliongezea Abuye
‘ungependa nikuite jina gani ulipendalo?’
‘Aaa!
Mimi lolote tu zuri utakalochagua wewe’
Waliendelea
na maongezi ya hapa na pale kuweza kufahamiana zaidi kadiri maongezi
yalivyozidi ndivyo na furaha ya Ashura ilizidi kuongezeka, Ashura alimsimulia Abuye
histora yake japo kwa ufupi, huu Ashura naye akiiskiliza historia ya Abuye
ndipo aligundua kuwa Abuye alikuwa ni mwanafunzi katika moja ya vyuo jijini Dar
es Salaam akisoma shahada ya sheria. Ashura alizidi kuvutiwa zaidi na Abuye aliyeonekana
na uwezo mkubwa wa kuongea na kujiamini. ‘hakika huyu ndiye mwanaume
anayenifaa’ aliwaza Ashura wakati akimsikiliza Abuye. Baada ya maongezi ya
takribani saa nzima Abuye alimwambia Ashura kuwa anaitaji kupumzika kidogo
kwani amechoka sana na pilika pilika za siku nzima
‘Ah!
Mbona mapema sana jamani, vipi umekula kweli hata?’ aliuliza Ashura kwa unyonge
kwani stori zilikuwa zimeshamkolea
‘Nimechoka
tu Ashura, nitakula nikiamka mida ya saa mbili’ alisema Abuye huku akijua wazi
kuwa Ashura asingependa amuache peke yake
‘sawa’
alijibu Ashura kwa unyonge ‘ukiamka uni text mwaya’
‘Ok
usijali nikiamka tu utakuwa mtu wangu wa kwanza kuwasiliana naye Ashura’
alijibu Abuye kwa uchangamfu jibu lililompa matumaini Ashura
‘Ok
baadae, sleep tight’ alijibu Ashura.
Baada
ya kujibu na kukata simu ilikuwa tayari ni mida ya saa 12 na dakika saba, Abuye
alijilaza kwa uchovu haikupita muda mrefu akawa tayari ameshachukuliwa na
usingizi.
Kwa
Ashura saa 12 ulikuwa ni muda wa kuangalia habari mbali mbali za kimataifa BBC
News Channel, ila kwa siku ile aliamua kujishuhulisha na shuhuli ambazo
angezifanya saa mbili usiku ili apate uda mzuri wa kuongea na Abuye, taratibu
ratiba yake ya kila siku ilianza kubadilika japo aliona kama jambo la kawaida
tu!, muda wote aliokuwa akijishuhulisha alimuwaza Abuye, aliiwaza sauti yake
akauwaza mwili wake uliokuwa si mfupi wala si mrefu sana unaweza kuuita mwili
wa kati si mnene sana wala si mwembamba pia, Ashura alizidi kutamani siku moja
auguse japo mara moja tu!. ‘Ah! Kajialiwa sauti sawa na mwili wake, jamani
duniani kuna wanaume ma handsome adi wa sauti’ aliwaza Ashura huku akitabasamu
Inaendelea...
DOWNLOAD HAPA! HUU MZIKI
MJUE ZAIDI:
Anaitwa Melissa michael kwa upande wa sanaa anajulikana kama Michy . Ni mwanafunzi wa sheria UDSM mwaka wa kwanza . Upcoming artist ambaye alituma demo yake katika studio za de fatality kilichopelekea kuonekana ana mwanga mzuri wa mziki na kupewa ofa ya kurekodi nyimbo yake mpya inayotambulika kama HUU MZIKI . Video ipo tayari chini ya utayarishaji wa director @Hanscana_ huku audio production ikisimamiwa na producer @mesenselektatz
SIKILIZA NA DOWNLOAD HAPA HUU MZIKI YA MICHY STAA MPYA KUTOKA DE FATALITY
DOWNLOAD HAPA! HUU MZIKI
MJUE ZAIDI:
Anaitwa Melissa michael kwa upande wa sanaa anajulikana kama Michy . Ni mwanafunzi wa sheria UDSM mwaka wa kwanza . Upcoming artist ambaye alituma demo yake katika studio za de fatality kilichopelekea kuonekana ana mwanga mzuri wa mziki na kupewa ofa ya kurekodi nyimbo yake mpya inayotambulika kama HUU MZIKI . Video ipo tayari chini ya utayarishaji wa director @Hanscana_ huku audio production ikisimamiwa na producer @mesenselektatz