Majuto alifunga ndoa na msichana mbichi
Tukio hilo limetokea Julai 8, mwaka huu pande za Mbagala Zakhem jijini Dar
ambapo mzee Majuto alifunga ndoa na msichana mbichi aitwaye Rehema Omary.
Mzee Majuto aliambatana na wasanii wenzake Suleiman Barafu aliyekuwa mpambe
wake na mwingine aliyefahamika kwa jina la utani kama mama Sharon.
Baada ya waandishi wetu kupata taarifa kuhusu tukio hilo, waliwahi kutia
timu Mbagala, nyumbani kwa binti huyo. Baada ya kufika, waandishi wetu
walibaini kuwa ni kweli kulikuwa na shamrashamra za ndoa ambayo ilikuwa
ikifanyika kwa siri huku watu wakizuiliwa kupiga picha.
0 comments:
Post a Comment