background img

The New Stuff

Sad news from KENYA

Sad news fro Kenya

Diamond Platnums akiwa ni miongoni wa abiria waliokwama kutokana na uwanja wa ndege wa Jomo Kenyata kulipuliwa leo alfajiri, ameiambia millardayo.com kwamba imebidi abiria wapelekwe hotelini na kuambiwa inawezekana ndege zikaanza kuruka saa moja au saa mbili usiku leo ambapo taarifa walizozisikia ni kwamba ni shambulio la bomu.
Kwa sasa imetangazwa abiria wako salama ambapo ndege zote zilizokua zinatua Nairobi zimeelekezwa kutua Mombasa.

KWA TAARIFA YAKO: Tarehe kama ya leo 07/08 mwaka 1998, Balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania zililipuliwa kwa milipuko ya mabomu. Ni miaka 15 imepita sasa.

Leo, tarehe 07/08/2013, Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta umekumbwa na janga kubwa la moto. Hizi ni tarehe mbili kubwa zenye historia kwa nchi ya Kenya.

Tunaungana na Wakenya kutoa pole kwa janga hili lililowakuta. Ungana nasi kutoa pole.
 
  source: milardaAyo,Facebook pages

0 comments:

Popular Posts