Staa wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja na mwanaye Paula Paul
Staa wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja na mwanaye Paula Paul wamekuwa
kama mtu na mdogo wake kutokana na kulingana vimo na kufuatana kila kona
kiasi cha kuzua maswali kwa watu.
Hivi karibuni wawili hao waliambatana kwenye mwaliko wa futari
iliyoandaliwa na msanii wa filamu, Aunt Ezekiel na kuwafanya mastaa wengine
kudhani ni mtu na mdogo wake.
“Ni vigumu kuamini kama huyu ni mwanao, miye nilipomuana nilidhani umekuja
na mdogo wako, kweli kuzaa mapema ni mali,” alisema msanii Devota Mbaga kwa
niaba ya wengine waliokuwa wakishangaa.
0 comments:
Post a Comment