background img

The New Stuff

RAU UNIT HISTORY PART 2

RAU UNITY THE MASHUJAA

          Hili ni kundi la muziki wa HIPHOP lililoanzishwa na wasanii wa muziki huo kutoka mtaa wa Rau, Moshi mjini.Kundi hili linajumla ya wasanii watatu Bambino,Baraka na Roger chini ya mwamvuli wa mtaa wa Rau.

CHIMBUKO LA RAU UNITY THE MASHUJAA:


Chimbuko la kundi ni msanii Bambino ambaye ndiye aliyekuja na wazo la kuanzisha kundi la mziki wa Hiphop RAU mwanzoni kundi lilitambulika kama MASHUJAA il baadae lilibadili jina na kuitwa RU UNITY THE MASHUJAA ikiwa ni lengo la kuitanua Hiphop Rau na kuimiza umoja kwa wasanii wa Hiphop Rau na Moshi kwa ujumla.

KAZI ZINAZOFANYWA NA KUNDI:

Kundi la RAU UNITY THE MASHUJAA linafanya kazi mbalimbali za muziki kazi hizo ni kama zifuatazvyo;

  1. Kundi linafanya Rapping au mziki wa kufokafoka

  2. Kundi linaandika mashairi ya nyimbo mbalimbali mf. Hiphop,Rnb

  3. Kundi linafundisha uandishi wa mashairi

  4. Kundi linafanya tafiti mbalimbali za kimuziki Tanzania

MTAZAMO AU MALENGO YA KUNDI;

Kundi lina mtazamo nwa kimapinduzi katika sanaa ya Tanzania.

Kundi lina malengo ya kuinua mziki wa Hiphop Moshi kwa kupitia kazi mbali mbali linazofanya.

VIKWAZO AU CHANGAMOTO;

Kundi linakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kukosekana kwa ushirikiano kutoka kwa wasanii wengine wanaofanya muziki

Vilevile kundi linakabiliwa na kuwepo kwa imani potofu miongoni mwa wanajamii juu ya muziki wa Kizazi kipya kuwa ni muziki wa kihuni

 AZIMIO:

Kundi limeazimia kukabiliana na vikwazo na changamoto zote zinalolikabili kwa kufanya harakati mbalimbali za kimuziki.

HITIMISHO:

Kundi linatoa pongezi kwa wadau wote wa muziki Tanzania kwa kuimarisha muziki nchini hususa muziki wa kizazi kipya pia kundi linatoa pongezi kwa wasanii mbalimbali wa HIPHOP Tanzania kwa kuisimamisha nguzo hiyo muhimu hapa nchini MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI SANAA.


0 comments:

Popular Posts