‘Salio lako jipya
ni Tsh. 200,050. Umepokea Tsh. 200,000 kutoka kwa 255652XXXXXXX-Ashura, kumbukumbu no. PP172XXXXXXXX.F5463XXXXX 30/01/2017’ Ni ujumbe ulioingia kwenye simu
ya Abuye huku akiilaani sauti ya sms iliyoingia alizidi kuuvuta usingzi
uliokuwa umemuelemea baada ya uchovu wa pilika pilika za siku nzima. Dakika si
nyingi si unaujua wasi wasi wa mtu aliyetuma pesa mahali alafu asipate jibu la
kupkelewa au la! Basi ndio wasi wasi uliompata Ashura ambaye wakati huo alikuwa
amejilaza kitandani kwake huku kanga moja ikiusitiri mwili wake uliopendezeshwa
na rangi nyeupe, mtoto wa kisambaa aliyekulia Tanga mjini akaanzisha maisha
yake jijini Dar es Salaam baada ya kupata kazi shirika moja la kimataifa. Ki
ukweli Ashura alijaaliwa maisha mazuri tangu utoto wake hakuijua shida, hakuwai
kuomba kitu akakikosa kwa wazazi wake ila dunia haina mwenyewe Ashura alikuwa
na njaaa moja tu! Njaa ya mapenzi. Haikuwa rahisi kuamini kama binti mrembo
kama Ashura angeweza kuwa na njaa ya mapenzi, vile alivyokuwa mrembo kila
mwanaume alimtamani na kuishia hapo hapo kumtamani kwani waliamini lazima
angekuwa mke wa kigogo Fulani na kumtongoza ni kujitafutia kifo mwenyewe.
Msitu
haukosi wanyama wakorofi, Abuye kijana wa Sinza wenyewe wanapaita Sinza kwa
wajanja Alisha ugusa moyo wa Ashura mchana wa siku hiyo. Ashura akiwa amejilaza
kitandani aliukumbuka mchana wake namna
ulivyokumbwa na mshituko wa furaha, ni akiwa ametokea Bank alipokuwa ameenda
kuonana na meneja wa bank ndipo alikutana na hali aliyombadilishia siku yake.
Akiwa anaelekea kwenye gari lake aina ya IST ghafla alitokea kijana ambaye hata
yeye hakujua alipotokea na kumwambia ‘dada umependeza’ ni maneno hayo mawili tu
yalitosha kumsisimua hadi kope za macho yake kwa mshangao uliochanganyika na
woga. Akionekana kama asiyejali yatokanayo na kauli yake Yule kijana
alimuangalia Ashura na kasha kutabasamu huku akielekea ndani ya bank.
Ashura
hakuacha kumtazama yule kijana huku akitingisha kichwa na kutabasamu alifungua
mlango wa gari na kuvuta pumzi ndefu huku ameshikilia usukani kwa mikono miwili
kama mtu aliyekuwa akijinyoosha viungo vya mwili. Hakuweza kuwasha gari muda
ule, alimtafakari Yule kijana kwa namna alivyokuwa na ujasiri uliojaa masihara kasha
akaitafakari kauli yake, dada umependeza, akatafakari ni lini mara ya mwisho
kuabiwa kauli kama hiyo hakika hakuikumbuka siku ya mwisho kuambiwa kauli ile,
akatabasamu ena huku akijichekesha mwenyewe na kujiandaa kuianza safari yake. Zilikuwa
zimeshapita karibu dakika 6 dakika zilizotosha kumfanya Yule kijana awe tayari
ametoka ndani ya ile bank, Ashura akiwa bize kutoa gari kwenye parking
alishaanza kumsahau Yule kijana hadi alipofika kwenye geti wakati akikabidhi
kikadi alichopewa na mlinzi getini ndipo akamuona Yule kijana akiwa amesimama
anaongea na boda boda.
‘Kaka
twende!’ ni sauti nyembamba nzuri ya mrembo ikitokea kwenye gari ilimuongelesha
Yule kijana aliyeonekana kama kuto kuijali sana huku akizidi kuongea na boda
boda.
‘Bro
sista ako anakuita kule’ alisema Yule boda boda kumwambia Yule kijana
‘Mpotezee
bhana mimi simjui ata’ alisema Yule kijana huku akiwa anachezea chezea ndevu za
kidevu chake. Baada ya kuisikia honi kutoka kwenye gari la Ashura Yule kijana
hakuwa na ujanja mwingine zaidi ya kumsogelea Ashura kwenye gari.
‘Kaka
mambo?, pakia kwenye gari mwaya’ alisema Ashura huku akitabasamu,
‘Asante
sista ila nipo na Yule boda boda’ alijitetea yule kijana,
‘Haya
sawa asante kwa kukataa lift yangu’ alisema Ashura kwa unyonge huku
akimuangalia Yule kijana, ‘Ah! Sista, usiwe mnyonge hivyo bhana unaupoteza
uzuri wako’ huku akiwa na tabasamu alimwambia Ashura huku akimdadisi zaidi. Akihisi
kama mapigo ya moyo yamebadilika Ashura alichukua pochi yake na kutoa kadi
yenye mawasiliano yake na kumpatia Yule kijana,
‘Mimi
naitwa Ashura, nipo pale UN, karibu siku moja kunitembelea’ alisema Ashura huku
akimkabidhi ile kadi.
‘Poa
sista mimi naitwa Abuye, baadae nitaku text upate namba zangu zinaishiwa na 52’
alisema Abuye akitabasamu.
Njiani
Ashura alizidi kumtafakari Abuye huku akijisemea mwenyewe Abuye uwahi kunitext
jamani’. Baada ya kufika ofisini Ashura alizidi kuisubiri sms ya Abuye kwa
hamu, kila ilipoingia sms aliiangalia kwa haraka hadi ilipofika mida ya saa
saba ilipoingia sms, ‘mamb vp sista, hii ndio namba yangu Abuye’. Huku akitabasamu
Ashura aliisave ile namba na kuijibu ile sms.
Inaendele...
0 comments:
Post a Comment