KUTOKA KIJIWENI__ETI TUNATAKA MZALENDO AMA WA DIGRII MBILI TATU..?__BOFYA HAPA KUJUA KULIKONI
NA MWANA KIJIWE
Habari za mchana mwenetu..? mimi kama kawada niko vizuri kabisa, najua umeshangaa kidogo vipi Zee leo nimeibukia kwenye siasa ila no sweti mtu wangu si unajua hata mimi ni mpiga kura..dah!! asikwambie mtu huku nako kunaitaji lugha yake ama wenyewe wanaita eti weledi.
enewei acha tuingie kwenye mishemihe zetu kijiweni leo si nilisema ngoja niende mitaa ya wale wanaojiita makamanda ama wanaharakati hapa town, kama nilivyo otea nikawakuta wanali-watch bunge la katiba kule dom!! nikasema yes ngoja Zee nile info za hawa maprezident tu bi hapa.
Si unanijua Zee zangu kutulia tuu mara nikasikia "mpumbavu huyu!!! anasema nini alaaa tena dokta" huyo alikuwa dogo mmoja hapa kijiweni kama kakimbia sana umri basi miaka twentiy faivu' hivi.
'haukamzi' dogo anatukana hawa waze uko mjengoni..?ila nikaona nisije ropoka nikaitwa mamluki
Sasa alichomtukania mjumbe huko dom ni eti ile ishu ya standard seven kuwa kigogo kule mjengoni
Zee nikana ndio mada iliyobamba apa kijiweni wadau wanabonga ya moyoni
nikamkumbuka mshikaji mmoja aliwahi kubonga kuhusu edukesheni za hawa waheshimiwa wetu ila kama alikuwa anawa diskasi sana wale jamaa wa maandamano eti wao aliyesoma sana ni yule mista advoket..?
samutaimu Zee nakubaliana na huyu mshikaji ila ngoja niulize swali wenyewe wanasemaga lakiwaki
"Mwenetu wewe ulitaka mbunge awe vipi..?" Zee nikamtupia dogo swali pale ghafla macho kama arobaini hivi yakanigeukia mtu mzima afu dizaini wakakuta na mimi nmeweka ule wanauitaga wamee!! kwani shingi ngapi babuu!
"Mi nataka awe jembe mzalendo mtetea ii nchi broo si hawa tumewapa nchi tangu uhuru adi leo amna kitu apa ni chadema ukawa mwanzo mwishoO!!"
dogo ile kamaliza kufunguka tu nikaona wana karibu wote wamemuunga mkono mwanao ikawa hivi yani "Eehh!! Ouyooooo hakuna kulalaaaaA!!! .... mpaka kielewekeeeeeE!!!"
Zee nikaona duh!! sasa hapa ishakuwa tabu wasije andamana niondoke buree ila mi si Zee? acha niwape busara ila vipi nitawakontroo awa raia nikaona ngoja niulize swali
Dogo wewe unaelimu ya kiasi gani...? dogo akanijibu kumbe ni student pale chuo kikuu chunguza chunguza zangu Zee nikagundua kumbe mdogo apa ni fomu six mmoja tena katokea kambi apa ana bonge la upara kwenye hedi katulia tuliii ni mjeda yule wa j
kujenga Ikonomi.
nikaona huyu nimwache apoze mikikimikiki ya jeshi nidili na hawa kaka zake kwanza,
Zee nikatoa zoezi dogo tu kwamba Oya masala tukachukueni makwanja tufyeke haya majani majani apa kijiwe si mnajua kuna yule mosikwito wa mchana ...wana wote wakagoma wanadai nani atawalipa kwa io kazi...afu Zee nikawauliza uzalendo wenu uko wapi sasa..?
weee!!! si kikanuka pale wacha watu waanze ropoka hovyo hovyo Zee nikajua kumbe hadi uku dawuni wako hivi hivi acha nijichenge zangu wasijeniletea ishu za kuandamana..
0 comments:
Post a Comment