Habari ni vipi mwenetu leo ni sandei nyingine tena ya huu mwaka 2014 ujue zisi yia umeenda fasta sana mwenetu! yani unaambiwa wana hapa kijiweni wanashangaa hivi wameshapiga ishu gani importanti hapa town wanaona hola tu!!. Mtu mzima si na mimi nikaanza kagua kale ka dayari kangu nione misheni zilizotiki mpaka nau! unaambiwa ni kama nusu ya mishe zote na mwaka ndio unaelekea ukingoni hau kamzi kila yia hatukamilishi mishe zetu wana..?
Basi wakati na thinki kwa nini huwa wana hatukamilishagi mishe zetu nyingi za maendeleo wazo likanijia hivi ni mishe gani ya kuapprochi motto mzuri iliyozingua hadi nau! unaambiwa kama zipo basi ni sifuri mwenetu asa mbona hizi zina tiki deile afu za mkwanja magumashi
Nikaona nisiwe mchoyo wa maarifa huyoo nikazama kitaa unaambiwa kizuri kula na ndugu yako na ndugu zetu si ndio wale wenetuwe mwenyewe mmoja wao mwanangu, ujue ishu za udugu haziwagi kwenye bladi tu! unaambiwa uduguni kokote mwenetu,
Basi mtu wako wa nguvu nikaibukia kijiweni pale nikakuta wana kibao unaambiwa nikatembeza gweraa!kwawana afu nkasikilizia michongo gani ilikuwa pale kijiwe, kama nilikuwa nao vile wana nao walikuwa wana diskasi ishu za maendeleo yetu kama vijana si unajua ndio ishu za msingi hizo town.
Ila wana wao walikuwa wanapanga michakato ya kupiga yani walikuwawanaweka mipango a mishe mishe si ndio mtu mzima nika introdjuzi mada yangu kuwa kwa nini mishe nyingi tunazozisukaga kila mwaka vijana hapa town hazi kamilikagi zote. Wana wakaanza kunipa sababu nyingi hadi nyingine nikawa sizijuagi ujue.
Mwana mmoja anakwambia maendeleo ni kama demu ujue sisi ma'boi huwa ndio tunao waapproachi watoto wa kike ila samu taimu huwa nao wakiona unazingua ndio wanakuibukia wenyewe asa maendeleo nayo ndio yako hivyo! mwenetu unaambiwa we suka miango yako gudi afu utaona mwenyewe yani unaambiwa mishe zisipo tiki basi utakuwa umeshaweka chaneli ya mishe nyingine kuwa gudi wenyewe wanasemaga zali!.
Ndio maana Zee huwa napenda kupozi na wenetu hapa kijiweni ujue hili ni fulu darasa we kama huamini fanya kutafta kijiwe mitaa ya kwenu hapo afu nenda kapozi na wana mkila stori mbili tatu za maisha afu urudi skani we mwenyewe utaniambia.
Jao ujue kuna wana wengine vijiwen huwa wanazinguaga ila mtu mzima mimi hao ndio siwafagiliagi kabisa yani unakuta boya napozi kijiweni twenty fo hawazi afu anakuja kugongea jero ya mihogo ya naiti ujue kuna kijiwe niliendaga Zee nikaona hawa wana ni maduanzi sana.
Asa mwenetu ngoja mi niende nikapige mishe mbili tatu nizidi sukuma hili gurudumu mbele tusomane mida mida mwenetu simulizi za shuga boy kama kawaida unaambiwa raundi hii mwenetu kafunguliwa bonge la duka pande za kino pale studio si umesha pasoma asa tukutane mida mida upate fulu mkasa mwenetu
0 comments:
Post a Comment