background img

The New Stuff

KUTOKA KIJIWENI__NIMWENDO WA ALTEZA ZILE FUMANIZI ZA USWAZI NI USANII WA BONGO MOVIE__BOFYA HAPA ZEE LIKUJUZE





 Asubuhi nyingine tena Zee ndo nimeamka mtu wangu na hang over ya hela kama mwanangu Joh makini wa kaskazini, fasta fasta bila kupoteza hizi sekunde naji flash ile kisela zee lionekane smart sharo si unajua dada zao tena.
Mjanja wa kitaa ni wakuwapitia pitia alau wawili watatu na utawapataje sasa mwenetu kwa mfano ndo wewe kivipi labda…? Anyway tuachane na ilo zogo ila zee linamaujanja yakutola wewe lifuate tuu wenyewe wanalitaga swagga boy.
Ila mwenetu vipi sasa michakato wa kutuia supu kwa mazaa pale kati ngoja Zee nikajenge mwili siunajua apa ni manyutrienti ndo mpango mzima babake’. Karibia mezani hapa mwanangu tuzikagulie mdomoni hizi chapatti za Azam.

Sasa hapo mzuka embu lipange dili hapa tukalichangamkie chapu chapu kuongeza uchumi wa Tz yetu, naanza kuikatiza mitaa ile kicheki bob kajua cha saa nne sasa naona nikatize huku uswazi sindio wanakokuita kwa wajanja wa town.
“Weweee!!! Kuwa makini fala wewe barabara za watu hizi hangaa shangaa tu!!” tobaa! Zee nikajirusha ile kininja ninja kufuata amri ya huyu bodaboda asijenigonga na tororoo lake bure, nilikua sijaamini wale wazee wa kwa mpemba walivyokua wakiwalaumu vijana wa huku uswazi asa leo ndo nimewajua japo kidogo.

Unajua ni nini Zee nilikua nashangaa..? ni huyu braza men mmoja apa yupo na sista du! Matata sana wenyewe huko town wanawaita visuu..unavijua wewe asa visu ni watotoama wachuda wazuri daka iyo toka kwa Zee ama ticha wako.
Mwanangu unazifahamu zile gari aina ya Alteza..? sasa ndo huyu braza men amelipaki hapa af kafungua mlango na bonge ya mziki unapiga tena ule wa Rick Ross mpya mpya hivi. Embu ngoja mwanetu ifanye ukachero kidogo..Alaa kumbe ichi ni kigrosari cha kishikaji ngoja Zee nijisogeze nimchekishie huyu mrembo wa braza men siunajua Zee mtu wa mitikasi taaluma nyingi asi vunga chalii.
Hawa wahudumu wako fasta kinoma yani kuvuta kiti tu uyu hapa “Kaka nikusaidie kinywaji gani…?” Zee kama niko ndotoni vile sauti nyororo imepenya kwenye ngoma ya sikio acha Zee nicheze Samba sasa. Siunaona mrembo saivi ni mida ya kazi naomba nisaidie Juisi baridi tropical siunajua Zee sina undugu na Bakhresa ila natupia bidhaa zake kinoma noma.
Juisi imeletwa tu Zee nikamtupia Yule mhudumu jicho zuri Zee kiboko kitu kikatabasamu kwanini na Zee nisitabasamu..? ila huyu namweka akiba kesho ntarudi tena. Huwa Zee sipendagi usumbufu nikachukua kimeo change nikaanza peruzi peruzi huu namchabo ule mrembo wa braza men.
Basi unaambiwa demu kamganda mchizi kama gluu zile asogezi jicho kando kudadeki, Ila Zee nikaona No sweti ngoja nivumilie kisela. Muda wa kama robo saa hivi ukapita Zee sijaona dalili ila yaliyokuwa yakiendelea hapa grosari ni fulu bongo movie unaambiwa demu kumbe ni kicheche kimoja kinakaa nyuma tu ya hapa grosari msela ndo anamaliza nacho mambo yake kimya kimya ila ni vipi vipi huyu mchizi kuchukua demu karunje kiivyo..? Zee lipo kazini hapa nazidi kula Info za huyu mrembo wa braza men toka kwa msela mmoja hapa grosari, usiulize nimejuana naye kivipi we jua Zee ndo ticha wako mtu wangu.
Kama mazabe Yule tozi akanynyuka kwenda wapi sijui Zee ndo nikaona yesi hi ndo chance waropa wanavyoitaga ile nataka kusimama tu mrembo akaniwahi huyoo akatoka kwenye gari kacheki cheki akapiga simu sijui alikuwa anabonga nini Zee nikatulia kwanza Yule mrembo kumaliza tu kuongea akarudi kwenye gari akatulia. Braza men akarudi kama dakika moja badae nikajua kumbe msela alikuwa ameenda msalani
Demu kampokea kwa mbwembwe kama kawa wakaendeleza mchezo wao mchana mchana. Dakika kama tano mbele nikaona demu kama kashituka hivi na msela naye ameshituka Zee nikajiuliza kulikoni pale kucheki kaunta kumbe kuna wasela wengine kama wanne hivi wamekuja pale wakaagiza vinywaji nao wakatulia dakika kama mbili tatu mmoja wao akasimama pale akanyooshea mkono lile Alteza la Braza men 

“Ndo huyu huwa anamchukua shemu broo!!” nikashituka kidogo vipi hapa fumanizi nini ama ndo sinema linaendelea “Huyoo huyooo!! huyoo!!” wasela hao kwenye gari la tozi demu naye akaanza kama kulia anaomba msamaha tena analia kabsa “mme wangu nisamehe ni amenitongoza tu” Braza men apo ni anatetemeka tena si kitoto ile kkubwa kabsa mwenetu.
Ikawa bonge la picha raia nao wakaanza leta wingu pale si unajua uswazi tena Zee nimekuwa mpole apa natafakari hau kamu!! Si nimepewa stori hapa huyu ni bonge la kicheche!!? Asa huyu msela kaniingiza Zee chakike leo nkamgeukia nianze kummaindi vipi mwenetu au ulitaka na mimi nifumaniwe nini…?
Msela akaniambia kuwa mpole kaka huu ni mchezo tu pale hakuna cha mume wala mke watu wako kazini pale .. Nkaona huyu naye ananiletea stori za Abunuasi hapa Zee nikarudisha macho kwenye fumanizi nikakuta Braza men keshahukumiwa siku mingi ni anahesabu vitita tu pale “Bado bado hazijafika laki tano”
Ndo nilichokisikia akisema mmoja wao pale Duh!! Braza men kapigwa parefu hivi. Ile kutoa tu wakamruhusu naye mbio kwenye gari lake mwendoo!!
“Kaka umeonazengwe hilo..?” ndo swali la msela baada ya braza men kusepa na Alteza lake demu akajifuta futa pale huku anabonge la tabasamu kwa wale masela, duh!! Nimeliona mwenetu kumbe si kila fumanizi ni laiv mengine bongo movie tu!!
Zee nikamchabo Yule demu hadi hamu ikapotea kabisa kwa Yule mhudumu nisijikutana na zengwe la braza men buree!!...ila Zee si ndiyo ticha wako huyu ngoja nitampitisha chocho zetu zile pale town adate mwenyewe ‘wani dei!!’
Zee ngoja nikapige lunch tusomane baadae mtu wangu!!

0 comments:

Popular Posts